Psalms 146

Kumsifu Mungu Mwokozi


1 aMsifuni Bwana!
Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.

Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,

2 cNitamsifu Bwana maisha yangu yote;
nitamwimbia Mungu wangu sifa
wakati wote niishipo.

3 dUsiweke tumaini lako kwa wakuu,
kwa wanadamu ambao hufa,
ambao hawawezi kuokoa.

4 eRoho yao itokapo hurudi mavumbini,
siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.


5 fHeri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,
ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,

6 gMuumba wa mbingu na nchi,
na bahari na vyote vilivyomo ndani yake:
Bwana anayedumu kuwa mwaminifu
milele na milele.

7 hNaye huwapatia haki walioonewa
na kuwapa wenye njaa chakula.
Bwana huwaweka wafungwa huru,

8 i Bwana huwafumbua vipofu macho,
Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao,
Bwana huwapenda wenye haki.

9 j Bwana huwalinda wageni
na kuwategemeza yatima na wajane,
lakini hupinga njia za waovu.


10 k Bwana atamiliki milele,
Mungu wako, ee Sayuni,
kwa vizazi vyote.

Msifuni Bwana.
Copyright information for SwhKC